Michezo

Yanga yaikalibisha Azam leo katika uwanja mpya wa Taifa.

.......................


KALAMA NYILAWILA KUVULIWA UBINGWA WA DUNIA IWAPO ATAPAMBANA NA FRANSIC


"Kama atataka kuzipiga na Francis Cheka tarehe 28 January 2012 badala ya kwenda kutetea ubingwa wake hilo siyo suala nitakaloingilia"

LAKINI NILIMUANDIKIA KAMANDA KOVA ILI AMPE MSAADA KWA AJILI YA MAZOEZI YA PAMBANO HILI LA UTETEZI NAYE ALIMUITA KARAMA NA FRANCIS MIYEYUSHO HIVYO SIPENDI KUHUSISHWA NA KUNYANG'ANYWA KWAKE UBINGWA MAANA KAMA MMOJA WETU AKIIDHINISHA TU PAMBANO KATI YA KARAMA NA CHEKA BASI UBINGWA UTAMTOKA MARA MOJA .

PST HAIWEZI KUTOA KIBALI CHA PAMBANO KATI YA CHEKA NA KARAMA KWA KUWA KUTOA KIBALI HICHO NI KUIDHINISHA KARAMA KUNYANG'ANYA UBINGWA WA DUNIA WA WBF. PST HAIFAHAMU LENGO LA PROMOTA KYANDO KULAZIMISHA PAMBANO AMBALO LITAMPOTEZEA UBINGWA MTANZANIA PEKEE MWENYE HADHI DUNIANI LINAPOHUSIKA SWALA LA MICHEZO.

HAKUNA MCHEZO WOWOTE AMBAO TANZANIA IMEFANYA VYEMA ZAIDI YA MASUMBWI YALIYOFANYWA NA KARAMA NYILAWILA.

NA IWAPO UBINGWA UATAMTOKA KWA NJIA YA KIJINGA NAMNA HII MAANA FRANCIS CHEKA YUPO HAPA HAPA TZ NA PAMBANO HILI LINAWEZA KUCHEZWA BAADA YA TAREHE 11 FEB 2012 BASI JUHUDI ZA KAMANDA KOVA KUULIPIA MKANDA HUO ZITAKUWA ZILIKUWA NI ZA BURE AIDHA KUMSADIA KWAKE KARAMA KWA HALI NA MALI ITAKUWA KAMA INA FULANI YA KUMTAPELI NA HIVYO PST HAIPENDI KUHUSISHWA NA HILI.

TPBO WAMEKWISHA KUTOA TAMKO LA KUTOMPA KIBALI PROMOTA KYANDO MPAKA BAADA YA PAMBANO LA UBINGWA HIVYO TPBC WAKIMPA KIBALI WAJUE WAZI KUWA WATAKUWA WAMEIDHISHA KARAMA KUNYANG'ANYWA UBINGWA WA DUNIA,



---------------------------------------

THIERRY HENRY ARUDI EMIRATES

Thierry Henry amekamilisha uhamisho wa muda mfupi kurudi Arsenal.

The Gunners wamekamilisha makubaliano ya bima na New York Red Bulls, kwa maana Henry sasa anaweza kuanza kuichezea Arsenal kuanzia Jumatatu katika raundi ya Kombe la FA dhidi ya Leeds.

The 34-year amesajiliwa kama mbadala wa Gervinho na Maroune Chamakh, ambao watakuwa wakielekea Africa kucheza CAN na timu zao za taifa Morocco na Ivory Coast.

Henry alisema: “Ni vigumu kuwa mkweli lakini linapokuja suala la Arsenal moyo ndio utakaokuwa unaongea.

“Tangu nilipojua the plan nyuma ya usajili wangu nilikuwa sawa na kurudi Gunners. Sijarudi Arsenal ili kuwa shujaa au ku-prove kitu chochote. Nimerudi kusaidia tu.

“Watu wanabidi waelewe kwamba Chamakh na Gervinho wanaenda kucheza CAN, hivyo niliitwa kuja kujaza gap waliyoiacha.”

Henry atavaa jezi namba 12 mpaka atakapomaliza mkataba wake wa miezi miwili.Welcome The Greatest King Theirry Henry.