Tuesday, March 6, 2012

NARGIS NA LULU WAFANYA KWELI

Kama kawaida ya kampuni yako ya RJ kufanya mambo makubwa katika tasnia yetu ya filamu safari hii imeamua kuwachezesha Elizabeth Michael (LULU) pamoja na Nargis Mohamed (NARGIS) katika mzigo mpya unaokwenda kwa jina la WOMAN WITH PRINCIPAL jamani ndani ya mzigo huu kinadada wamefanya mambo makubwa sana kama kawaida yangu mimi sina maneno mengi ngoja wenyewe mtajionea mambo, Mwaka huu ni mwaka wa mabadiliko mtaona vitu vingi vipya.

Pozi kabla ya shooting kuanza huyu ndiye Nargis anakuja kwa kasi mpya kabisa baada ya sinema ya Yellow Banana alikaa kimya sana kwa muda mrefu sasa amesema amerudi kufanya mambo ya ukweli



Huyu ndiye Lulu baada ya kufanya nae sinema ya Family Disaster movie iliyoongoza kwa mauzo mwaka jana sasa amerudi na WOMAN WITH PRINCIPAL

Peace

 Kama kawaida ya Lulu kwa mapozi

 Nargis katika scene ya mahakamani, alicheza kama Hakimu ndani ya mzigo huu

 Ofisini kwake


Full shangwe

Makini katika kazi


Kama kawa makamuzi yanaendelea


On Set


Mbwembwwe tena za Lulu

Akiwa na Camera Man wangu Farid Uwezo

11 comments:

DM wa Shinyanga. Kakake Johari na rfk wa Nelly wa Tabata said...

Kaka nakukubali sana, kazi zako nzuri. Nadhani una maanisha A WOMAN WITH PRINCIPLES na sio PRINCIPAL

Anonymous said...

Acha kupark au kukaa barabarani ww na washamba wenzako ipo siku mtaokota maiti na vilema,

Anonymous said...

Ray hiyo Title ya movie ikisomeka " A woman with principle" italeta maana zaidi ya "Woman with principal"
neno principle na principal yanatamkika sawa lakini maana ni tofauti.

emuthree said...

Kazi nzuri mkuu, tupo pamoja

weprac said...

Me huyo lulu jamani ivi huwa anaogea maji ya bongo kweli,mtoto anawaka kama tanzanite,du kweli Mungu kuumba.

Anonymous said...

Hiyo siyo peace symbol mzee ni fuckoff,peace symbol palm inakuwa imetuangalia ss

Anonymous said...

hello ray, hongera kwa kaz nzuri mnajitahidi. Nashauri msione garama kuajiri watu wa kufanya proof reading tittle za movie zenu na subtitles kwenye movies maana ni aibu kwa watu wanaopitia na kuona mnavoandika broken english. wabongo wengi tuko poor in english lakini kwavile hii ni kaz ajiri mtu uone utakavo improve hata mauzo!halafu kama movie ni ya kiswahili basi tittle ziwe kiswahili, kama humo ndani mmetumia kiingereza 80% ndo muipe tittle ya english.inashangaza tittle ya english content purely swahili, haileti maana! Tittle ya hii should read 'A woman of principles' and not as you've written

Anonymous said...

Nargis ni mwanamke mzuri sana. Ana natural beauty na ana mvuto sana. Anaweza kuigiza, namshauri ajiingize moja kwa moja kwenye fani na ajiheshimu na kuheshimu kazi, yeye ni mke wa mtu na mama wa mtoto.

khalidi athumani said...

kaka ray big up sana mrembo nargis wa ukweli sana na umefanya kazi nzuri kaka yangu mie najua kwamba wewe sio mtu wa kubahatisha unatoa vitu vya ukweli sana mie nausubiri mzigo huu wa principal kwa hamu kubwa nakutakia kazi mafanikio katika kazi yako achana na watu wenye kuleta majungu we piga kazi.

Anonymous said...

nice to see you the girl under 18!!!! i mean LULU

Unknown said...

Kaka ray big up sana